Akithibitisha
kukamatwa viongozi hao kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan
Mungi alisema kuwa viongozi hao walikamatwa kwa mahojiano kutokana na
kutoa kauli hatarishi kwa amani wakati wa mkutano wao uliofanyika katika
uwanja wa Mwembetogwa kwa ajili ya mabaraza ya ukusanyaji wa maoni ni
rasmu ya katiba.
Kamanda
Mungi alisema kuwa kibali ambacho Chadema walipewa kilikuwa kikianza saa
9 Alasili hadi saa 12 .;00 ila wao waliendelea na mkutano huo hadi
majira ya saa 12 .25 na kila walipofuatwa zaidi ya mara moja kuelezwa
kuhusu muda wa kibali chao kuisha bado viongozi hao waliendelea
kuendesha mkutano huo huku wakitumia vipasa sauti kutoa maneno ya
dhahaka dhidi ya jeshi la polisi
Sunday, 25 August 2013
TAARIFA ZA KUKAMATWA VIONGOZI WA CHADEMA IRINGA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment