Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Kagera, Bi. Constansia Buhiye leo amesisitiza kuwa
maamuzi yaliyotolewa na Halmashauri kuu ya Mkoa ya kuwafukuza na
kuwaondolea nyadhifa madiwani wanane wa chama hicho Manispaa ya Bukoba
yako palepale.
Akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa CCM
kuhusiana na Tamko la Katibu Mwenezi Taifa Ndugu
Nape Nnauye la kutengua maamuzi ya Halmashauri kuu ya Mkoa wa Kagera,
Bi Buhiye amesema hata taarifa ya Nape hajaisikia, na kwamba maamuzi
waliyoyafanya ni kwa mujibu wa Katiba ya Chama.
Mwenyekiti
wa CCM mkoa Kagera akiongea na waandishi wa habari leo kususitiza kuwa
maamuzi ya halmashauri kuu ya mkoa dhidi ya madiwani wanane wa CCM
Bukoba yako palepale
Waandishi wa habari wakisikiliza maelezo ya mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera leo
0 comments:
Post a Comment