Wafanyabiashara
ya maziwa ya ngamia kutoka katika
jamii ya Borana wakifungasha maziwa kwa ajili ya kutiwa
katika majokofu huko Isiolo. Kuanzia mwezi Septemba,
serikali itatoa mikopo isiyo na riba kwa wanawake na
vijana kuanza au kuboresha biashara zao.
jamii ya Borana wakifungasha maziwa kwa ajili ya kutiwa
katika majokofu huko Isiolo. Kuanzia mwezi Septemba,
serikali itatoa mikopo isiyo na riba kwa wanawake na
vijana kuanza au kuboresha biashara zao.
Fedha
hizo, zitakazojulikana kwa jina la "Mfuko wa Uwezo", mwanzo zilitengwa
kwa ajili ya uwezekano wa kufanya duru ya pili ya uchaguzi wa rais baada
ya uchaguzi mkuu wa mwezi Machi.
Wakati wa
kuzinduliwa kwake tarehe 19 April, Rais Uhuru Kenyatta alitangaza
kwamba serikali itaanzisha muundo wa kupanga tena malengo ya fedha hizo
kufaidisha makundi hayo mawili ndani ya kipindi cha kwanza cha siku 100
ofisini, ambacho kiliisha tarehe 18 Julai.
"Tunatoa
wito kwa vijana na wanawake wote kuwa tayari kwa mikopo hiyo," Makamu wa
rais William Ruto alisema tarehe 28 Julai, akitangaza kutolewa mwezi
Septemba. "Hatutawatoza riba yoyote hivyo wasiwe na uoga wa kuomba fedha
hizo."
Mbunge wa
Garissa Adan Duale alisema tarehe rasmi ya kutolewa itatangazwa Agosti,
pamoja na wabunge wanawake wa kaunti na wabunge wa majimbo watakaofanya
kazi kama wasimamizi wa pamoja wa mfuko huo.
Kamati za
Mfuko wa Maendeleo ya Majimbo zitakuwa wasimamizi wa mfuko huo hadi
kamati tofauti zitakapoundwa kwa ajili ya mfuko wa Uwezo, alisema.
"Kuchelewa
kutolewa kwa fedha hizo kulitokana na uanzishaji wa muundo wa namna ya
kutolewa fedha hizo," aliiambia Sabahi, akiongezea kwamba waombaji
wanaweza kutuma maombi ya mikopo kupitia kwenye majimbo yao, ambayo
yatapokea fedha hizo kutoka serikali kuu.
Vikundi
vya vijana wapatao kumi wenye umri kati ya mika 18 hadi 36 lazima
viwasilishe mpango wa biashara kustahili kukopa hadi shilingi 500,000
(dola 5,720), Duale alisema. Masharti kwa waombaji wanawake yatakuwa
hayo hayo, lakini pasipo kikwazo cha umri.
Waombaji watatakiwa kulipa asilimia 3 ya kiasi cha mkopo katika ada za kushughulikia maombi, alisema.
"Kurejesha
mkopo kutoka kwa mtu mmoja mmoja ni vigumu zaidi kuliko kurejesha
kutoka kwa kikundi," alisema, akiongeza kwamba marejesho yatawezesha
fedha kuwanufaisha watu wengi zaidi. "Mkopo lazima urejeshwe ili wale
ambao hawakunufaika katika utoaji fedha wa kwanza waweze kunufaika
katika utoaji unaofuatia."
Rachel
Shebesh, mwakilishi mwanamke kutoka Kaunti ya Nairobi, alisema fedha
zitasaidia kuongeza ukuaji wa uchumi kwa kuwawezesha wanawake na familia
zao.
"Vijana
na wanawake ni zaidi ya asilimia 60 ya idadi ya watu. Kwa kuwawezesha,
Dira ya 2030 ya nchi itafanikishwa," aliiambia Sabahi, akiongeza kwamba
Mfuko wa Uwezo utaongezea fedha zilizopo kama vile Mfuko wa Maendeleo ya
Shughuli za Vijana na Mfuko wa Shughuli za Wanawake.
Justus
Mochere, mwenye miaka 33, mweka hazina wa Kikundi cha Vijana cha
Mwamanua katika Kaunti ya Kisii, alisema kikundi chake kimetuma maombi
kwa Mfuko wa Uwezo ya shilingi 200,000 (dola 2,300) kupitia eneo la
ubunge la Kitutu Chache.
Alisema
Kikundi cha Vijana cha Mwamanua kinataka kuanzisha ufugaji wa kuku na
kupanua mradi wa ufugaji wa samamki ambao unaendeshwa kwa zaidi ya mwaka
mmoja.
"Tumekuwa
tukiepuka kuomba mikopo kutoka katika mifuko mingine kwa sababu ya
kizuizi cha riba inayotozwa, lakini Mfuko wa Uwezo usio na riba ni mzuri
kwetu," aliiambia Sabahi. "Tunatarajia kuuongeza na kusaidia familia
zetu."
Mkaazi wa Garissa Abdikadir Hassan Abdi, mwenye miaka 29, alisema anatarajia fedha zitagawanywa kwa haki.
"Baadhi
ya kamati ambazo zitasimamia Mfuko wa Uwezo awali zilikuwa na
upendeleaji," alisema. "Kama kamati zitaendelea na mwelekeo wake wa
upendeleo na ubaguzi, itakuwa njia ya kuleta wasiwasi kwa jamii, vita
vya kikabila na kushindwa kwa mfuko huo."
0 comments:
Post a Comment