Mgeni
Rasmi katika Mpambano wa Kimataifa wa kuwani Mkanda wa Ubingwa wa Dunia
wa WBU,kati ya Mabondia Francis Cheka wa Tanzania na Phil Williams wa
Marekani,Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella
Mukangala (mwenye koti jeupe) akimvisha Mkanda wa Ubingwa huo,Bondia
Francis Cheka baada ya kumshinda kwa Point Mpinzani wake,katika Mchezo
uliomalizika usiku huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es
Salaam.Kulia ni Bingwa wa Zamani wa Masumbwi,Fransous Bhotha.
Bondia
Francis Cheka wa Tanzania (kushoto) akimrushia makonde makali mpinzani
wake,Phil Williams kutoka nchini Marekani wakati wa mpambano wao wa
Kimataifa kuwania Mkanda wa Ubingwa wa Dunia wa WBU,uliofanyika usiku
huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es Salaam.Bondia Francis
Cheka ameibuka kidedea baada ya kumchapa mpinzani wake huyo kwa Point.