Wednesday, 27 August 2014

Vyama vya Siasa kukutana na Rais Kikwete kuhusu Katiba Mpya



Vyama vyote vya siasa nchini vinatarajiwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete kabla ya mwisho wa wiki hii, kujadiliana na kushauriana juu ya maendeleo ya mchakato wa Katiba mpya. 

Vyama hivyo vya siasa vitakutana na Rais kwa mwavuli wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na vitakutana siku yoyote kuanzia leo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana juu ya kikao hicho, Mwenyekiti wa TCD ambaye pia ni Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo alisema baada ya kukutana Agosti 23 mwaka huu, viongozi wa vyama hivyo walikubaliana kukutana na Rais Kikwete, ndipo walipomuandikia barua ya kumuomba akutane nao na Rais akawajibu kuwa atakutana nao kabla ya mwisho wa wiki hii.

Vyama hivyo vya siasa ni pamoja na vinavyounda kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambavyo ni CUF, CHADEMA, NCCR-Mageuzi ambavyo viongozi wake wamethibitisha kushiriki. Vingine ni CCM, TLP, UDP na UPDP inayowakilisha vyama visivyokuwa na wabunge.
Alipoulizwa Cheyo ni mara ngapi wamejaribu kukutana na Rais Kikwete alisema: 
“Mimi nimeshangaa Rais kutukubalia kwani hii ni mara ya kwanza kumuomba na yeye amekubali na kusema kabla ya mwisho wa wiki hii atakutana nasi.”
“Hii ilitokana na viongozi wa vyama vya siasa pamoja namambo mengine kuazimia kutafuta nafasi ya kuonana na Rais Kikwete kwa lengo la kushauriana naye na Mwenyekiti waTCD (Cheyo) niliwasiliana naye na kuomba nafasi ya wajumbe wa TCD kuonana naye.” 
Mwandishi alipomtafuta Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, ambayeni sehemu ya UKAWA, James Mbatia, alisema:
“Sisi tunakwenda kukutana na Rais (Kikwete) kama TCD na hiyo imetokana na azimio la 16 katika mkutano uliofanyika Februari 12 na 13 mwaka huu, ambapo tuliazimia kuwa TCD iendelee na maridhiano ili kupata Katiba bora.” Chanzo WAVUTI

0 comments:

Post a Comment