Mkandarasi Mkuu anayeshughulikia mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini
Dar es Salaam, Strabag International ametangaza kufungwa kwa muda
kipande cha barabara ya Mandela hadi makutano ya Ubungo Mataa.
Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Yahya Mkumba amesema kipande cha barabara ya Mandela kuanzia makutano ya barabara ya Morogoro upande wa kushoto uelekeo wa Tabata kuanzia Ubungo Mataa hadi Darajani patafungwa kuanzia tarehe 25/08/2014 mpaka tarehe 30/08/2014 ili kupisha ujenzi.
Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Yahya Mkumba amesema kipande cha barabara ya Mandela kuanzia makutano ya barabara ya Morogoro upande wa kushoto uelekeo wa Tabata kuanzia Ubungo Mataa hadi Darajani patafungwa kuanzia tarehe 25/08/2014 mpaka tarehe 30/08/2014 ili kupisha ujenzi.
Watumiaji wa barabara hiyo watalazimika kutumia upande mmoja wa barabara
hiyo. Magari yatakayokuwa yanatokea Mwenge, Kimara na Shekilango
yatalazimika kutumia barabara ya upande wa kulia ambayo pia itakuwa
ikitumika na magari yanayotoka Tabata kuelekea Ubungo.
“Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaotokea,” alisema Bw. Mkumba. Chanzo WAVUTI
“Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaotokea,” alisema Bw. Mkumba. Chanzo WAVUTI
0 comments:
Post a Comment