Wednesday, 11 September 2013

Angalia Picha za Mwandishi wa The Citizen ajeruhiwa kwa Mapanga mkoani Singida

 

DSC02917
Mwandishi wa habari wa gazeti la The Citizen na mwananchi mkoani Singida, Awila Silla amenusurika kuuawa na mtu anadhaniwa kuwa Jambazi baada ya kukatwa katwa kichwani na kusababisha kuzirai. Tukio hilo limetokea juzi saa mbili usiku jirani na mahakama ya mwanzo ya Utemini mjini Singida. Awila ambaye amelazwa wodi 2  hospitali ya mkoa amedai baada ya kukutana na kijana huyo aliamuriwa kutoa Fedha na baada ya kudai hana, jibu hilo lilisababisha kijana huyo kuanza kumkata Mapanga na alipoangauka na kuzirai alinyang’anywa  simu yake ya  kiganjani .Hata hivyo Awila amedai kuwa bado hajatoa taarifa ya tukio hilo polisi

0 comments:

Post a Comment