Tuesday, 3 December 2013

JE WAJUA KUWA NGUCHIRO NDIYE MNYAMA BINGWA WA KUUA NYOKA NA ANAE MUOGOPA COBRA?


Nguchiro-Jangwa


Na Lwitiko Peter 
JE WAJUA?
Nguchiro bingwa wa kuua nyoka anayeogopa cobra

NGUCHIRO ni mnyama mdogo jamii ya panya, anayepatikana kwa wingi barani Afrika na kusini mwa mabara ya Ulaya na Asia.

Kuna kama jamii 33 hivi za nguchiro. Lakini kuna jamii nyingine nne za ziada ambazo hupatikana huko Madagascar.

 Hawa ni jamii ndogo ya Galidiinae. Awali, jamii hizi nne ziliwekwa katika kundi la wanyama wengine wanaopatikana huko Madagascar lakini baadaye ikaja kujulikana kuwa wana sifa tofauti, hivyo kuundiwa makundi yao yanayojitegemea.

Utafiti wa kijenetiki unaonyesha kuwa Galidiinae wana uhusiano wa karibu na wanyama wengine wa familia ya Eupleridae, ambao wanakaribiana sana na nguchiro.

Mwonekano

Kama tulivyodokeza hapo juu, nguchiro hupatikana kwa wingi katika maeneo ya Afrika na kusini mwa Ulaya na Asia. Lakini pia kwa kiasi kidogo hupatikana huko Puerto Rico na sehemu ya visiwa vya Caribbean na Hawaiian.

Lakini huko walipelekwa kama wanyama wa kufugwa na kupambana na wanyama waharibifu na hatari kama vile panya na nyoka.

 Kuna jamii kuu 33 za nguchiro ambao kwa wastani ukubwa wao ni kati ya futi moja na nne kwa urefu. Uzito wa nguchiro unatofautiana sana kulingana na jamii husika.

Wapo nguchiro wadogo ambao uzito wao ni kama gramu 280 tu wakati wapo wengine wakubwa ambao hufikia uzito wa zaidi ya kilo nne.

 Baadhi ya jamii ya nguchiro huishi maisha ya upweke huku kila mmoja akijitafutia chakula chake mwenyewe.

0 comments:

Post a Comment