Nguchiro-Jangwa
|
Na Lwitiko Peter
JE WAJUA?
Nguchiro bingwa wa kuua nyoka anayeogopa cobra
NGUCHIRO ni mnyama mdogo jamii ya panya, anayepatikana kwa wingi barani Afrika na kusini mwa mabara ya Ulaya na Asia.
Kuna kama jamii 33 hivi za nguchiro. Lakini kuna jamii nyingine nne za ziada ambazo hupatikana huko Madagascar.
Hawa ni
jamii ndogo ya Galidiinae. Awali, jamii hizi nne ziliwekwa katika kundi
la wanyama wengine wanaopatikana huko Madagascar lakini baadaye ikaja
kujulikana kuwa wana sifa tofauti, hivyo kuundiwa makundi yao
yanayojitegemea.
Utafiti wa
kijenetiki unaonyesha kuwa Galidiinae wana uhusiano wa karibu na wanyama
wengine wa familia ya Eupleridae, ambao wanakaribiana sana na nguchiro.
Mwonekano
Lakini huko walipelekwa kama wanyama wa kufugwa na kupambana na wanyama waharibifu na hatari kama vile panya na nyoka.
Kuna jamii
kuu 33 za nguchiro ambao kwa wastani ukubwa wao ni kati ya futi moja na
nne kwa urefu. Uzito wa nguchiro unatofautiana sana kulingana na jamii
husika.
Wapo nguchiro wadogo ambao uzito wao ni kama gramu 280 tu wakati wapo wengine wakubwa ambao hufikia uzito wa zaidi ya kilo nne.
Baadhi ya jamii ya nguchiro huishi maisha ya upweke huku kila mmoja akijitafutia chakula chake mwenyewe.
0 comments:
Post a Comment