Tuesday, 9 September 2014

Hongera UKAWA. Hakuna kurudi nyuma tena - Mwl Lwaitama

Maoni ya Mwalimu Lwaitama kuhusu maamuzi yaliyofikiwa katika mkutano baina ya Rais Kikwete na Wajumbe wa TCD.
Hongera UKAWA kwa kufanikisha hili lakini kazi bado mbichi!. Bado ni lazima kuelewa kuwa makubaliano haya yamehalalisha kuwepo kwa Rasimu mbili za Katiba inayopendekezwa, ile iliyowasilishwa Bunge Maalum na Jaji Warioba kwa niaba ya Tume ya Rais ya Mabadiriko ya Katiba kama Rasimu ya Pili ya Tume hiyo ya Rais na Rasimu ya CCM itakayotokana na Bunge Maalum lilosusiwa na UKAWA kuendelea hadi tarehe 4 Oktoba kuchakachua maudhui ya kimapinduzi yaliyomo katika Rasimu ya Pili iliyotayarishwa na Tume ya Rais.

UKAWA sasa tekelezeni dhana ya 'UKAWA ndio mpango mzima' !!! Lazima
kuwaeleimisha na kuwahamazisha wananchi kukataa Rasimu ya CCM (iliyosheheni mambo ya ajabu ya Bunge 3 Serikali 2!)) na kuhakikisha kuwa Serikali Kuu ya na Bunge la Jamhuri ya Muungano litakalopatikana baada ya Uchanguzi wa Oktoba 2015 itakuwa Serikali na Bunge litakalo kuwa limesheheni wanasiasa wenye nia dhabiti ya kujadili, kuboresha na kupitisha Rasimu ya Pili ya Katiba iliyowasilishwa Bunge Maalum na Jaji Warioba kwa niaba ya Tume ya Rais ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Warioba.

Lazima Bunge litakalo patikana baada ya Uchanguzi Mkuu wa 2015 liwe Bunge litakalo rekebisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu Wajumbe wa Bunge Maalum kuwa nusu theluthi moja wanasiasa na theluthi mbili wajumbe waliochanguliwa na makundi husika ya kiraia kuingia Bunge Maalum na Tume ya Rais ya Mabariko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Warioba kuendelea kusimamia mchakato wa katiba ndani ya Bunge Maalum na wakati wa upigwaji wa kura ya maoni ( kwa kutoa elimu ya uraia) hadi katiba mpya ipatikane. hongera UKAWA. Hakuna kurudi nyuma tena. Umoja wa vyama vya NCCR, CUF na Chadema utabadilisha siasa Tanzania kiasi kikubwa na ukiritiba wa chama kimoja, chama dola, kisiasa, utakomeshwa.
Mwl. Lwaitama
Maoni ya Mwalimu Lwaitama akiwaandikia Wanazuoni (kundi pepe la majadiliano). Chanzo WAVUTI

0 comments:

Post a Comment